SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, April 16, 2011

WASANII WA FILAMU WAKUTANA NA MHESHIMIWA RAIS NYUMBANI KWAKE

Ujumbe wa Wasanii wa Filamu uliopo mjini Dodoma umefanikiwa kukutana na Mheshimiwa Rais Dr Jakaya Mrisho Kikwete nyumbani kwake.Ujumbe huo ukiongozwa na Jacob Stephen(JB) na Wasanii wengine akiwemo Vincent Kigosi,Steven Kanumba,Single Mtambalike,Jackline Wolper,Zuena Mohamed na Odama umeweza kuwasilisha kile kilichowaleta hapa Dodoma hasa kipindi hiki cha Bunge kuwasilisha dhamira yao ya kutangaza Amani ndani ya nchi yetu.Ujumbe huo wa Amani ulipokelewa vizuri na Mheshimiwa Rais na akasema kuwa atakuwa nasi bega kwa bega kwa suala hili kwani Amani si kitu cha kuchezea kabisa.Sisi kama Wasanii tunafurahi sana na tunakupa pongezi kubwa Rais wetu kwa kutupokea vizuri na kuukubali ujumbe wa kutangaza Amani Nchini

Ray na Mheshimiwa Rais Dr Jakaya Kikwete

Odama akipata picha na Rais

Kanumba akiwa na Mh Rais Dr Jakaya Kikwete

Jackline Wolper akipata picha na Rais

JB akiwa na Mh Rais Dr Jakaya Kikwete

Richie akipata picha na Mh Rais Dr Jakaya Kikwete

Steven Nyerere akipata picha na Mh Rais Dr Jakaya Kikwete
chanzo:BOFYA

0 comments:

Post a Comment