
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudentia Kabaka
akitoa tamko la Serikali kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya
usitishwaji wa utaratibu wa kukodisha wafanyakazi unaofanywa na baadhi ya
mawakala binafsi wa huduma za ajira wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi
wa idara ya habari(MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam.
--
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA KAZI NA AJIRA

1.Wizara ya Kazi na Ajira imekua ikipokea malalamiko toka kwa wadau mbalimbali utaratibu wa udalali wa kukodisha wafanyakazi
katika makampuni unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira
nchini.



