Watoto
wa marehemu Medard Kabikile Stima, aliyekuwa Mweka hazina wa Manispaa
ya Ilala wakiwa wamebeba msalaba pamoja na picha kuongoza shughuli ya
kuaga mwili wa marehemu baba yao katika viwanja vya Karimjee jijini Dar
es Salaam, jana na baadaye maziko yalifanyika makaburi ya Kinondoni.
Marehemu
Stima alifariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea Julai 31, 2014
karibu na eneo la Bwawani, wakati wakielekea mjini Morogoro kwa shughuli
za kikazi, wakiwa na gari aina ya Landcluiser Mali ya Manispaa ya
Ilala, ambapo lilipasuka gurudumu la mbele na kuacha njia na kugonga mti
uliokuwa pembeni ya Barabara. Marehemu Stima alifariki dunia wakati
akipatiwa matibabu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Dereva
anaendelea na matibabu.
Familia ya Marehemu Medard Kabikile Stima katika shughuli ya kuaga mwili.
Meya mpya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi akitoa heshima zake za mwisho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia akitoa heshima zake za mwisho.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa nae alikuwa mstari wa mbele kutoa heshima zake.
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh.Raymond Mushi ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki akitoa heshima yake.
Waombolezaji wakitoa heshima zao za mwisho.
Kila mmoa alikuwa na sura ya majonzi.
Mwanamitindo Flaviana Matata alikuwa ni miongoni mwa waombolezaji.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Rugimbana (wa pili kulia) alikuwa ni mmoja ya waombolezaji.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI), Hawa Ghasia (Katikati) akiwa na viongozi wengine.
Mwanamitindo Flaviana Matata akimmfariji mke wa Marehemu Stima.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia akitoa heshima zake za mwisho.
Familia ya Marehemu Stima ikiongozwa na Mama Stima wakiwa na nyuso za majonzi.
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh.Raymond Mushi ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki akitoa machache.
Meya mpya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi akitoa salamu za rambirambi.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mwandisi Mussa Natty akitoa salamu za rambi rambi.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akieleza wasifu wa marehemu Stima.
Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Elizabeth Nyambibo akieleza machache.
Msemaji
wa Familia akitoa shukrani zake za pekee kwa watu wote walioweza
kufanikisha maziko ya ndugu yao Marehemu Stima. PICHA ZOTE NA CATHBERT
KAJUNA.
0 comments:
Post a Comment