SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, April 14, 2014

MATUKIO KATIKA PICHA LEO ASUBUHI BUNGENI DODOMA

1Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Tundu Lissu akiwasili leo kuhudhuria kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye Ukumbi mjini Dodoma.

4Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakiwasili leo kuhudhuria kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye Ukumbi mjini Dodoma.
5Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Philemon Ndesamburo (kulia) naProfesa  Kulikoyela Kahigiwakiwasili leo kuhudhuria kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye Ukumbi mjini Dodoma.
9Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Ismail Jussa (kushoto),Macharo Othman Said(katikati) na Nassor Ahmed Mazrui wakiwasili leo kuhudhuria kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye Ukumbi mjini Dodoma.10  Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta akitoa ufafanuzi  kwenye kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye leo mjini Dodoma.
11Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Tundu Lissu akiwasilisha maoni ya wachache  leo kuhudhuria kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo kwenye Ukumbi mjini Dodoma.12Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Anne Makinda (kushoto) na Pandu Ameir Kificho(kulia) wakifuatilia mjadala kwenye kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo leo mjini Dodoma.
13Mwenyekiti wa Kamati namba sita wa Bunge Maalum la Katiba Stephen Wassira akiwasilisha maoni ya Kamati yake leo mjini Dodoma kwenye kikao cha ishirini na mbili cha Bunge hilo.
Picha na Bunge Maalum la Katiba

=======

KAULI ZILIZOTOLEWA BUNGENI LEO NA TUNDU LISSU, WASSIRA, MTIKILA NA ISMAIL JUSSA

Zifuatazo ni kauli zilizotolewa na viongozi mbalimbali wa zile kamati kwenye bunge la katiba linaloendelea sasa hivi hapa Dodoma ambapo viongozi hawa leo April 14 2014 wameendelea kuwasilisha taarifa kutoka kwenye kamati zao,
Ni maoni ya pande mbili ambazo ni maoni ya wengi ambao ndio wanaounga mkono serikali mbili alafu maoni ya wachache ambao wanaunga mkono uwepo wa serikali tatu.
Tundu Lissu: ‘Nusu karne ya uongo iishe, Tanganyika iliuwawa na amri za Mwalimu Nyerere na hakuwa na mamlaka kisheria kuiua, hatujawahi kuwa nchi moja, habari ya Tanzania kuwa nchi moja iliingizwa ktk katiba miaka 20 baada ya muungano, nchi hii ni haramu…. miaka 50 ya kudanganyana ikome, nchi hii inahitaji kuelezwa ukweli’

Mchungaji Mtikila: ‘tulijengwa kwenye misingi ya uongo ndio maana Mungu alishindwa kubariki hii nchi yetu kwa miaka 50, uongo tuuondoe, swala la muungano lilikua utapeli wa kisiasa, tuurudie ukweli kuhusu uhuru wa Watanganyika na Wazanzibari’

Mh Wassira: ‘Hati ya Muungano ipo, naahidi kwa niaba ya Jamuhuri itawasilishwa kwa Mwenyekiti ndani ya siku mbili zijazo, kama Wananchi wangetoa maoni kutaka kuvunja muungano, je tume ingeyaleta? serikali 3 italeta mgongano’

Mh Wassira: ‘Katiba ya Znz ndio itabakia kuwa sheria kuu kwa Znz kwa mambo yasiyokua ya muungano, tukiweka serikali 3 hapa zikaweka masharti kuna watu watapata matatizo, itapunguzia Wazanzibari fursa’

Ismail Jussa: ‘Hoja za historia kwamba tulikua vipi haziwezi kulibakisha taifa katika mgando, ukiangalia katiba ya muda ya mwaka 1965 inaendelea kuitambua Tanganyika na kuwepo makamu wawili wa Rais’

Ismail Jussa: ‘Mkataba wa muungano haukutoa mamlaka kwa chombo chochote kubadilisha kilichopo ndani, ajabu bunge limefanya, tunapokua Znz tunasema mengine tukija huku tunaufyata, Wazanzibari watatuhukumu’

Ismail Jussa: ‘Zanzibar tumeachwa watupu, tumechoka na hatukubali tena, ktk mfumo wa serikali mbili Zanzibar haitaweza kujisimamia kamwe, hatutakubali kuendelea nao’

Ismail Jussa: ‘Kama kuna nia njema kwa nini kuna kufichaficha, mfano mwingine hai ni Rais wa Znz kuondolewa kuwa makamu wa Rais’

CHANZO: MILLARDAYO.COM