SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, April 10, 2014

Kamati mbalimbai zawasilisha maoni yao uchambuzi wa sura ya kwanza na sita ya Rasimu ya Katiba Mpya

2a
Mwenyekiti wa Kamati namba mbili (2) Shamsi Vuai Nahodha akiwasilisha maoni ya wajumbe wa Kamati yake leo mjini Dodoma juu ya uchambuzi wa sura ya kwanza na sita ya wa rasimu ya Katiba mpya.
7b
Makamu  Mwenyekiti wa Kamati namba tano Assumpter Mshama akiwasilisha maoni ya wajumbe wa Kamati yake leo mjini Dodoma juu ya uchambuzi wa sura ya kwanza na sita ya wa rasimu ya Katiba mpya.
6
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Bunge hilo leo mjini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa Sura ya Kwanza na Sita wa rasimu ya Katiba mpya.
3
Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakifuatilia uwasilishaji wa maoni ya wanakamati mbalimbali upande wa Sura ya kwanza na sita wa rasimu ya Katiba mpya leo mjini Dodoma.
4
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Pandu Ameir Kificho (kushoto) na Balozi Seif Ali Idd(kulia) wakijadiliana jambo leo mjini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa sura ya kwanza na sita wa rasimu ya Katiba mpya unaofanywa na Kamati mbalimbali.
5
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba January Makamba (kushoto) na Dkt. Asha Rose Migiro (kulia) wakijadiliana jambo leo mjini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa sura ya kwanza na sita wa rasimu ya Katiba mpya unaofanywa na Kamati mbalimbali.
8
Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakiwasili leo kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya kusilikiliza uwasilishaji wa sura ya kwanza na sita ya rasimu ya Katiba mpya.(Picha na Bunge Maalum la Katiba).