Issa Musa
Timoth Conrad - Mtayarishaji na mtunzi.
--
CLOUD 112 ATUHUMIWA KUIBA CREDIT ZA FILAMU YA DOKTA
MAX.
: AISAMBARATISHA KAMPUNI YA TIMAMU EFFECTS
Kampuni iliyokuwa inakuja kwa kasi katika tasnia ya
filamu Timamu Effects ambayo inamilikiwa na Jackson Kabirigi na Timoth Conrad
au maarufu kwa jina la Tico inasemekana kuwa imesambaratika kutokana na kile
kilichoitwa kuwa ni hujuma kwa mmojawapo wa wamiliki hao.
Akizungumza na mtandao huu kwa masharti ya kutotajwa
jina lake, msanii mmoja ambaye pia alishiriki katika kuigiza filamu hiyo
alifunguka kuwa chanzo cha kusambaratika kwa kampuni hiyo ni kitendo cha Tico
ambaye alikuwa mpigapicha na mhariri wa filamu hiyo kuandika kuwa filamu hiyo
imeongozwa na Issa Musa au Cloud 112 ambaye ni prodyuza wa muvi hiyo badala ya
Jackson Kabirigi ambaye ndiye aliongoza filamu hiyo.
Inasemekana kuwa baada ya kuona kosa hilo Jackson Kabirigi ambaye anang’ara na filamu ya
Kisate alimkabili Tico kumuuliza kulikoni lakini badala ya Tico kufanya
marekebisho alisema kuwa yeye anafuata alichoambiwa na Cloud 112 jambo ambalo
ni kinyume na kanuni za filamu duniani kote kwa mtu kumpa sifa asiyestahili.
Baada ya majibizano makali kati ya wamiliki hao
inasemekana kuwa kila mmoja aliamua kushika yake wakiiacha kampuni iko hewani.
Mtoa taarifa wetu aliyejibainisha kuwa anamkubali sana
Kabirigi alienda mbali zaidi kwa kudai kuwa huo ulikuwa ni mpango ambao tayari
ulishawekwa toka awali katika kumhujumu Kabirigi baada ya kuonekana kung’ara katika upande wa
uongozaji wa filamu hasa baada ya filamu aliyoiongoza ya Mdundiko kushinda tuzo
kadhaa za kimataifa.
FC ilijitahidi kuwapata Jackson Kabirigi na Timoth
Conrad bila mafanikio ila ilifanikiwa kuwasiliana na wasanii Wastara na Hidaya
Njaidi ili kujua ukweli kuwa ni nani aliyeongoza filamu hiyo kati ya Jackson
Kabirigi aliyeandikwa kama ‘2nd Director’ na Issa Mussa Cloud 112 aliyeandikwa
kama ‘Director’ ambapo walifunguka kama
ifuatavyo,
Wastara alisema
‘’Sinema iliongozwa na Jackson Kabirigi sijui wenyewe walivyoamua, ‘’Pia aliulizwa mwigizaji mwingine ambaye ni Hidaya Njaidi naye alifunguka hivi
“Director
ninayemjua ni Jack ambaye aliongoza filamu hiyo, kwani Cloud alikuwa na scene
nyingi za kuigiza hata kuna wakati ambao
Jack alikuwa anamwelekeza akimwambia siyo hivyo fanya hivi na Cloud kutii kama
jina la muongozaji kaandikwa yeye itakuwa ajabu labda
walisaidiana,”anasema Hidaya Njaidi
Bado FC inawatafuta wahusika wakuu wa habari hii,
Jackson Kabirigi na Timoth Conrad. Ili kuweka sawa jambo hilo sambamba na
mtayarishaji mkuu wa filamu hiyo maana siku hizi suala la Credit katika sinema
linatumika vibaya.
*Habari hii imeletwa hapa na Myovela Mfwaisa
CHANZO: NA H@KI NGOWI
0 comments:
Post a Comment