SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, May 26, 2013

Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Amjulia Hali Sheha wa Shehia ya Tomondo Zanzibar Baada ya Kumwagiwa Tindikali na Watu Wasiojulikana

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohammed Shein akimuangalia Sheha wa Shehia ya Tomodo wilaya ya Magharibi Unguja, Mohammed Said Kidevu (kulia) jinsi alivyoathirika na tindikali aliyomwagiwa na mtu asiyefahamika. Bw. Kidevu alimwagiwa tindikali hiyo juzi alipokuwa akirudi nyumbani kwake kutoka kuchota maji; amelazwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar. Kushoto ni Dkt. Salim Mohammed.
Bw. Mohammed Kidevu, Sheha wa Shehia ya Tomondo, Zanzibar (kulia) akimuelezea Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein jinsi alivyomwagiwa tindikali hiyo. Bw. Kidevu alimwagiwa tindikali hiyo juzi na mtu asiyefahamika akielekea nyumbani kwake akitoka kuchota maji. Wa pili kulia ni kaka wa Bw. Kidevu, Sudu Mgeni Said

0 comments:

Post a Comment