SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, April 18, 2012

MAKAMU WA RAIS DK. GJARIB BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA DINI LA WAISLAMU NA WAKRISTO JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo lililoanza leo Aprili 18, kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Viongozi wa Dini wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, alipofika kufungua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo, lililoanza leo Aprili 18, 2012 kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini alipowasili kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam,kwa ajili ya kufungua Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo, lililoanza leo Aprili 18, 2012.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Viongozi wa dini baada ya kuzindua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo katika Hoteli ya White Sands, jijini Dar es Salaam, leo Aprili 18, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya Viongozi wa Dini, baada ya kuzindua rasmi Kongamano la Dini la waislam na Wakristo, katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam, leo Aprili 18, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais.

0 comments:

Post a Comment