SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, July 8, 2011

Saa Chache Kuelekea Uhuru Sudan Kusini

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
South Sudan flag 
Sudan Kusini inahesabu saa chache ili kuwa Taifa jipya kabisa kuzaliwa duniani Jumamosi ya Julai 9.Rais wa Sudan Omar al-Bashir na wageni wengine mashuhuri kutoka kote duniani watahudhuria sherehe hizo zitakazofanyika katika mji mkuu Juba.Zaidi ya asilimia 99 ya Wasudan Kusini walipiga kura kujitenga na Sudan Kaskazini katika kura ya maoni iliyofanyika mwezi Januari.Kura hizo ni sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2005 kumaliza miongo miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyosababisha watu 1.5 milioni kufa.Nchi mpya ya Sudan itakuwa na utajiri wa mafuta lakini itakuwa moja ya nchi maskini kabisa duniani kutokana na mapigano ya muda mrefu.Sherehe zitaanza baada ya saa sita usiku saa za Sudan (2100 GMT) kwa kuhesabu dakika chache kufikia saa kamili ya kuwanza kwa siku wakitumia saa kubwa katikati mwa Juba.Mwandishi wa BBC Will Ross anasema katika kuelekea kwenye tukio hilo la kihistoria, vituo vya redio vimekuwa vikipiga wimbo mpya wa Taifa la Sudan Kusini.
Mapema wiki hii Bw Bashir aliahidi kuiunga mkono Sudan Kusini na kusema kuwa anataka Taifa hilo jipya kuwa ‘salama na lililotengamaa."Tutawabariki ndugu zetu wa Kusini nchini mwao na tunawatakia mafanikio" alisema Bw Bashir, aliyekubaliana na mkataba wa amani na chama cha Sudan People's Liberation Army (SPLA).Lakini ameonya kuwa ‘Uhusiano wa kindugu’ utategemea na mipaka salama na kutoingilia masuala ya nchi jirani (Kusini au Kaskazini)"Kwa hiyo tunafuraha sana na tunashukuru kwa mchango ao kwa Taifa hili."Rebecca Garang, mke wa hayati John GarangKulikuwa na wasiwasi huenda vita vingezuka tena baada ya mapigano mapya ya hivi kribuni katika maeneo ya mpakani Abyei na Kordofan Kusini ambayo yalilazimisha watu 170,000 kukimbia makazi yao.Hata hivyo makubaliano tofauti ya wiki za hivi karibuni na kuondoa vikosi kwenye mipaka kumerejesha hali ya utulivu.Rebecca Garang, mke wa hayati John Garang aliyeongoza waasi wa Sudan katika vita vya wenyewe kwa wenyewe , ameiambia BBC kuwa watu wake hawana matatizo na watu wa Kaskazini isipokuwa serikali yao."Kuna rafiki zetu wengi tu ambao walikufa wakati w vita lakini tuko hapa kwa ajili ya damu yao," alisema.
For more: Click 

0 comments:

Post a Comment