Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea katika hafla ya chai ya jioni
iliyoandaliwa na Mke wa Waziri Mkuu wa Malaysia Datin Paduka Seri Rosmah
Mansor maaulum kwa wake wa viongozi nyumbani kwake Putrajaya Malaysia.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete (kushoto ) akiongea na baadhi ya wake wa
viongozi wa kitaifa kutoka nchi za Afrika wakati walipokaribishwa kwenye
hafla ya chai ya jioni na mke wa Waziri Mkuu wa Malaysia Datin Paduka
Seri Rosmah Mansor (kulia) nyumbani kwake Putrajaya Malaysia. (.Pichani
akifuatiwa wa pili kulia) ni Mke wa Makamu wa Rais wa Kenya Mama Pailine
Kalonzo pamoja na mke wa Waziri Mkuu wa Lesotho Mama Mathato Mosisili
(wa tatu kutoka kulia).
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete pia Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA (kushoto)
wakibadilishana mawazo Juni 22,2011 na mke wa Waziri Mkuu wa Lesotho
Mama Mathato Mosisili (nguo ya mistari) pamoja na mwenyeji wao Mke wa
Waziri Mkuu wa Malaysia Datin Paduka Seri Rosmah Mansor (kulia) nyumbani
kwake Putrajaya Malaysia. alipowaalika kwenye chai ya jioni.(Picha na
Mwanakombo Jumaa-MAELEZO).
*****************************
Na Anna Nkinda – Putrajaya, Malaysia.
Wake
wa viongozi wa Afrika wameshauriwa kutunza mahusiano yaliyopo baina yao
ili waweze kushirikiana kwa pamoja kutatua matatizo yanayowakabili
wanawake na watoto katika nchi zao kwani kundi hili limesahaulika kwa
kiasi kikubwa katika jamii.
Ushauri
huo umetolewa jana na Mke wa Waziri Mkuu wa Malaysia Mama Datin Paduka
Seri Rosmah Mansor alipokuwa akiongea na wake wa viongozi kutoka nchi
za Tanzania, Lesotho, Kenya na Zambia wakati walipomtembelea nyumbani
kwake Putrajaya kwa ajili hafla ya chai ya jioni.
Alisema
kuwa moja ya malengo ya kazi zao ni kuhakikisha kuwa kina mama na
watoto wanaishi katika mazingira salama hivyo basi kama wanataka
kufanikiwa zaidi jambo la muhimu ni kufanya kazi kwa pamoja na
kubadilishana mawazo waliyonayo kwani Afrika ni moja na changamoto
zinazowakabili wanawake na watoto zinafanana.
“Kazi
mnazozifanya zinafanana na kuna malengo ambayo mmejiwekea ili muweze
kufanikisha kazi zenu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa kina mama na
watoto wanaishi katika mazingira salama hivyo basi ni lazima muungane na
kuwa kitu kimoja hakika kwa kufanya hivi mtaweza kumkomboa mwanamke na
mtoto wa kiafrika”, alisema Mama Mansor.
Mama
Mansor aliendelea kusema kuwa kutokana na uhalisia ni rahisi kwa
wanaume kujiangalia wao wenyewe na kutatua matatizo yao lakini kwa
wanawake na watoto wanatakiwa kupewa uangalizi wa ziada na msaada wa
lazima hasa kwa wale wanatoka katika familia maskini.
Akiongea
kwa niaba ya wenzake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alisema kuwa wao
kama wake wa viongozi wanakazi kubwa ya kuhakikisha kuwa kinamama na
watoto wanapata huduma muhimu katika jamii ikiwa ni pamoja na elimu na
afya.
Mama
Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo
(WAMA) alisema kuwa kwa upande wa Tanzania amekuwa akijitahidi
kuhakikisha kuwa watoto wa kike ambao ni yatima wanapata elimu na vifo
vya kina mama wajawazito na watoto vinapungua.
“Taasisi
yangu ya WAMA imesaidia katika jitihada za Serikali kuhakikisha kuwa
vifo vya kina mama wajawazito na watoto vinapungua kwa kuchangia vifaa
vya afya katika Hospitali, vituo vya Afya na Zahanati na kutoa elimu kwa
jamii kupitia kampeni mbalimbali za uhamasishaji”, alisema Mama
Kikwete.
0 comments:
Post a Comment