Rais Yoweri Museveni.
Rais Yoweri Museveni wa Uganda leo analihutubia taifa katika ukumbu wa bunge kuzungumzia masuala muhimu na msimamo wan chi hiyo.
Hotuba
kama hiyo hutolewa mara moja katika mwaka kila mwanzoni mwa mikutano ya
bunge, na hutolewa kuzungumzia suala lolote lenye umuhimu kwa taifa.
Rais
huyo atazungumzia masuala mbali mbali ikiwemo kutoa ufafanuzi juu ya
suala la kukua kwa uchumi, kuongezeka kwa gharama za maisha na mfumuko
wa bei.
Waziri
wa Habari Mary Karooro Okurut amesema rais Museveni ataelezea suala la
nishari na mtandao wa barabara ikiwa ni pamoja na elimu na sekta ya
afya.
Amesema
rais pia atazungumzia mapungufu yaliyopo katika utoaji huduma katika
sekta za elimu na afya, na kuongezea kuwa sehemu kubwa ya ahadi
zilizotolewa mwaka jana zimetimizwa.
Mwaka
jana rais Museveni aliahidi kukua kwa kasi kwa uchumi, kuimarishwa kwa
vita dhidi ya rushwa na kujenga bwawa la kuzalisha umeme la Bujagali
litakalozalisha MegaWati 250.
WAKATI HUO HUO
Rais Yoweri Museveni amewatahadharisha mawaziri wapya nchini humo dhidi ya tabia ya majivuno.
Amesema
tabia hiyo ni moja ya mambo yanayosababisha kuvunja umoja miongoni mwa
makada wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM).
Aidha amefafanua kuwa aliangalia kigezo cha uwezo wa upatanishi na kujenga umoja wakati akiunda baraza jipya la mawaziri.
0 comments:
Post a Comment