SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, May 10, 2011

Umoja wa mataifa waelezea hali ya wasiwasi Syria

Umoja wa Mataifa umeelezea wasi wasi kuhusu hali ya usalama katika mji wa Deraa Kusini mwa Syria, huku serikali ya nchi hiyo ikiendeleza mkakati wake wa kuwasaka wapiganaji wa waasi.
Umoja wa mataifa, umesema shirika lake la kutoa misaada, halijaruhusiwa kufika mjini humo na kuwa shirika lingine la kutoa misaada halijafanikiwa kupokea dawa na vifaa vya matibabu kuwasaidia wakimbizi wanaotoroka mapigano kati ya wanajeshi wa serikali na waasi.
Hakuna mawasiliano katika mji wa Deraa kwa muda wiki mbili sasa baada ya serikali ya nchi hiyo kutuma wanajeshi na vifaru ili kujaribu kutwaa udhibiti wa mji huo kutoka kwa wapiganaji wa waasi.
Wakati huo huo, muungano wa Ulaya EU umetangaza kuiwekea Syria marufuku ya kuagiza silaha.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa muungano huo, serikali ya nchi hiyo haitaruhusiwa kuagiza silaha au vifaa ambavyo vinaweza kutumiwa kukandamiza upinzani.
Maafisa 13 wa ngazi ya juu wa serikali ya Syria na washirika wao, pia wamepigwa marufuku kusafiri nchi 27 za muungano huo na amana zao zilizoko katika nchi za Ulaya zimezuiliwa.
****************************
WAKATI HUO HUO
Mkuu wa idara ya kutoa misaada wa Umoja wa Mataifa Valerie Amos ametoa wito wa kusitishwa kwa muda mashambulio yanayofanywa Libya ili kupunguza mgogoro wa kibinadamu unaoendelea nchini humo.
Baroness Amos aliliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kwamba Misrata, ngome pekee inayoshikiliwa na waasi magharibi mwa Libya, iko katika hali mbaya na inakabiliwa na upungufu wa chakula pamoja na maji.
Takriban watu 750,000 wameikimbia Libya tangu ghasia kuibuka dhidi ya uongozi wa Kanali Muammar Gaddafi.
Wakati huo huo, majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya, Nato yamefanya mashambulio kwenye mji mkuu Tripoli, ikiwa ni harakati kali kufanyika katika wiki kadhaa zilizopita.
Ripoti zinasema majengo manne yalilengwa, likiwemo eneo la familia ya Kanali Gaddafi, shirika la kijeshi la kijasusi na makao makuu ya kituo cha televisheni ya taifa.
Serikali ilisema ofisi ya tume ya watoto nchini humo ilishambuliwa, na watoto wanne walijeruhiwa.
Imekuwa vigumu kuthibitisha taarifa hizo.
Huko Misrata, waasi wanasema wamefanikiwa kusogeza majeshi ya serikali.
Mji huo umezingirwa na majeshi yanayomtii Kanali Gaddafi kwa miezi miwili sasa.
Na bbc swahili.

0 comments:

Post a Comment