SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, April 21, 2011

UFUNGUZI WA JENGO LA MAMLAKA YA BIMA ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya usimamizi wa Bima,(TIRA) Prof Gamaliel Mgongo Fimbo,alipohudhiria katika sherehe za ufunguzi wa jengo la ofisi za mamlaka ya usimamizi wa Bima Tawi la Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohamed Shein ,akisalimiana na Naibu Kamisha wa Bima Zanzibar,Juma Juma Makame,alipohudhiria katika sherehe za ufunguzi wa jengo la ofisi za mamlaka ya usimamizi wa Bima Tawi la Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la ofisi za mamlaka ya usimamizi wa Bima (TIRA) Tawi la Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohamed Shein, akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Jengo la ofisi za mamlaka ya usimamizi wa Bima Tawi la zanzibar jana, Kilimani Mjini Zanzibar.

Miongoni mwa maafisa wa mamlaka ya usimamizi wa Bima wakiwa katika sherehe za ufunguzi wa jengo la ofisi za mamlaka hiyo Tawi la Zanzibar,ufunguzi wa jengo ulifanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohamed Shein.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohamed Shein,akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi za mamalaka ya usimamizi wa Bima Tawi la Zanzibar,wakati wa sherehe za uzinduzi wa jengo la mamlaka hiyo jana huko Kilimani Mjini Zanzibar,(kushoto) Waziri wa Fedha,Uchumi na Mipango ya Maendeleo,Omar Yussuf Mzee,(kulia)Kamishna Mkuu Isarael L.Kamuzora na Mwenyekiti wa Bodi Prof Mgongo Fimbo.
Picha na Ramadhan Othman, Ikulu Zanzibar
Na Othman Mapara

0 comments:

Post a Comment