SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, April 28, 2011

BUNGE UGANDA LAPITISHA BAJETI YA MATUMIZI YA ZAIDI YA SH. TRILLION MOJA

Bunge la Uganda.
Bunge nchini Uganda limepitisha matumizi ya ziada ya shilingi trilioni 1.7 kwa ajili ya kununua ndege (Fighter Jets) na shilingi bilioni 2.8 kwa ajili ya shere za kuapishwa kwa rais, pamoja na upinzani mkali liliokumbana nao kutoka kwa wabunge wa upinzani.
Wakijadili ripoti ya kamati ya Bajeti kuhusu matumizi ya ziada, wabunge kadhaa wa upinzani wamepinga matumizi hayo na kuapa kutohusika katika kupitisha ripoti hiyo.
Waziri kivuli wa kambi ya upinzani Oduman Okello amejaribu kulishawishi bunge hilo kupunguza bajeti hiyo kutoka shilingi bilioni 2.8 hadi shilingi bilioni 1.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, serikali ya Uganda inataka kuridhiwa kwa matumizi ya shilingi bilioni 2.8, bajeti ya ziada ya maendeleo ya shilingi trilioni 1.468 na ziada ya mapitio kwa mujibu wa sheria ya shilingi bilioni 56, inayofanya jumla ya bajeti ya ziada kufikia shilingi trilioni 1.54.
Na.Mo Blog.

0 comments:

Post a Comment