SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, May 27, 2010

Shirika la Amnesty latoa ripoti ya mwaka

LONDON
Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International linasema ulimwengu haufanyi juhudi za kutosha kuendeleza haki, huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na hujuma, mateso na umaskini. Katika ripoti yake ya mwaka kuhusu haki za binadamu duniani, shirika hilo limezilaumu serikali mbalimbali kwa kuzuia maendeleo katika kulinda haki za binadamu kwa kukataa kujiunga na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ya ICC mjini The Hague Uholanzi, au kwa kuwalinda washirika wao wasifikishwe mbele ya vyombo vya sheria. Shirika la Amnesty International limezikosoa Urusi na China kwa ukiukaji wa haki za binadamu. Limemkosoa pia rais wa Marekani Barack Obama kwa kushindwa kuifunga jela ya Guantanamo. Shirika hilo limesema mwaka wa 2009 ulikuwa muhimu kwa haki ya kimataifa kwa sababu mahakama ya ICC ilitoa waranti wa kukamatwa rais wa Sudan Omar Hassan al Bashir kwa uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.
Deutsche Welle.

0 comments:

Post a Comment