Mwenyekiti na Wajumbe wateule
Mamlaka ya wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Maliasili na
Utalii, Mhe. Balozi Khamis Suedi Kagasheki (MB) (wapili kutoka kulia kwa
waliosimama msitari wa mbele) mara
baada ya kuzinduliwa rasmi katika Ukumbi wa Ngorongoro ulioko Makao
Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es salaam
Wenyeviti
na Wajumbe wateule wa vyombo vitatu, Bodi ya Leseni za Biashara za
Utalii Tanzania, Mamlaka ya Rufaa na Kamati ya Ushauri wa Kitaalam
wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Balozi Khamis Suedi Kagasheki (MB) (wanne kutoka kulia kwa waliosimama
msitari wa mbele) mara
baada ya kuzinduliwa rasmi katika Ukumbi wa Ngorongoro ulioko Maqkao
Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es salaam.
--
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Khamis Suedi Kagasheki (MB)
ametangaza kuanza rasmi kwa msako wa wafanyabiashara wa sekta ya utalii
(makanjanja) wanaofanya biashara kinyume na taratibu.
Akizungumza
katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Leseni za Biashara za Utalii
Tanzania, Mamlaka ya Rufaa na Kamati ya Ushauri wa Kitaalam vya Wizara
alisema, serikali imeamua kupambana na wafanyabiashara wa sekta ya
utalii wanaoikosesha mapato kwa kufanya biashara hiyo kinyume na
taratibu.
“Leo
ninazindua Bodi ya Leseni za Biashara za Utalii Tanzania inayoundwa na
watu makini, watu ambao hawawezi kusukumwa na rushwa ndogo ndogo ili
kuziba mianya yote ambayo inasababisha serikali kukosa mapato. Hivyo
kupitia bodi hii, sasa mfanyabiashara na serikali wote watapata faida,”
alisema Mhe. Kagasheki.
Aidha
aliongeza kuwa, hivi sasa leseni nyingi zimekwisha muda wake na hivyo
wafanyabishara wanalazimika kuomba upya na hapo ndipo vyombo hivyo vipya
vitakapoanza msako kwa kutekeleza majukumu yake ya kusaidia katika
usimamizi, kutoa miongozo na ushauri wa kitaalam kulingana na sera na
sheria.
Mhe.
Kagasheki aliongeza kuwa, kuundwa kwa vyombo hivyo ni suluhisho katika
kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya utalii nchini.
Na Haki Ngowi
Na Haki Ngowi
0 comments:
Post a Comment